The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Global Voices inakusanya, inapanga na kuyapaza maongezi ya kwenye mtandao - inaangaza mwanga kwenye sehemu na watu ambako vyombo vingine vya habari mara nyingi hupasahau


2010-03-26

Pakistani: Vitendo vya Unyanyasaji Watoto Vyaongezeka

Msemo 'Unyanyasaji watoto' hutumika kueleza vitendo vya aina mbalimbali vilivyo jinai na vinavyofanywa dhidi ya watoto. Wanablogu wanajadili vitendo hivi vya unyanyasiaji watoto vinavyokera na vinavyozidi kuongezeka nchini Pakistani.

2010-03-24

Ghana: tamasha la Twestival 2010 Mjini Accra: Shughuli Yenye Maana?

Kama uanahabari wa kijamii unabadilisha mtindo ya mawasiliano katika nchi za Magharibi, basi kwa hakika haujapungukiwa katika kufikia sehemu zinazovutia barani Afrika. . Kwa hiyo haishangazi kwamba MacJordan, wa Global Voices, anashirikiana na Rodney Quarcoo ili kulifikisha tukio hili la kuburudisha kwa watu wa Ghana.

2010-03-23

Mali: Vitambaa Vyasuka Nguzo za Uchumi na UtamaduniVideo post

Kwa kupitia video, tunaona na kujifunza kuhusu umuhimu wa utamaduni na ongezeko la kiuchumi ambalo utengenezaji vitambaa huwapa baadhi ya watu na mashirika nchini Mali. Vikundi vya wanawake, wasanii na watalii wote wananufaika na utamaduni huu wa kutia rangi vitambaa na upakaji rangi kwa kutumia matope.

2010-03-21

Middle East & North Africa

“Mfanyakazi wa ndani anapotoroka kutoka kwenye nyumba ya mwajiri wake, kituo cha polisi hakiwezi kufanya lolote kwa sababu hakuna sheria dhidi ya wafanyakazi wa ndani wanaotoroka. Kwa hiyo ofisa wa kituo cha polisi anamwambia mwajiri wa ki-Lebanoni aseme kuwa (mtoro huyo) aliiba pesa,” anaandika Ethiopian Suicides.

Uganda: Wanafunzi Wacharuka, Kampala Yawaka Moto

Jumanne, majanga mawili tofauti yaliikumba Kampala, mji mkuu wa Uganda: wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Makerere walifanya ghasia baada ya wanafunzi wenzao wawili kupigwa risasi. Na makaburi ya Kasubi, ambayo ni sehemu ya Urithi wa Dunia ya UNESCO na eneo la kaburi la mfalme wa moja ya makabila makubwa zaidi ya Uganda, liliteketea kwa moto.

Misri: Wafanyakazi wa IslamOnline Wagoma

Mamia ya wafanyakazi, wahariri, na waandishi wa habari walianza mgomo wa kuonyesha hasira yao katika mtandao unaosomwa sana wa jiji la Cairo unaojulikana kwa jina la Islamonline baada ya kuwa wafanyakazi wapatao 250 wamefukuzwa kazi. Kwa mara ya kwanza, wagomaji wanatumia kwa ufanisi na vizuri kabisa aina mpya ya chombo cha habari ili kuvuta usikivu na uungwaji mkono katika kile wanachokipigania, kuanzia na Twita inayoendelea mpaka mmiminiko wa habari wa hapo kwa hapo.

2010-03-17

Afrika Kusini: Ubaguzi wa Julius Malema

Wakati tabia za Rais Jacob Zuma zimekuwa zikizua mijadala mikali na yenye uhai katika ulimwengu wa blogu wa Afrika Kusini, hivi sasa ni mwanasiasa mwenye utata ambaye pia ni rais wa Umoja wa Vijana wa ANC, Julius malema ambaye anatengeneza vichwa vya habari. Hivi karibuni, aliwaongoza wanafunzi katika kuimba wimbo wa zamani wa kupinga ubaguzi wa rangi unaoitwa Ua Kaburu.

2010-03-16

Mwaka Mmoja Baada ya Mapinduzi, Viongozi wa Madagaska Wakabiliwa na VikwazoPhotos post

Machi 17, 2009 nchini Madagaska, vikwazo vinavyowalenga viongozi wa sasa wa Madagaska vinaandaliwa kwa kushindwa kwao kuheshima makubaliano ya Maputo ambayo hapo awali yalifikiwa na pande zote zinazohusika. Matokeo ya vikwazo hivyo ni pamoja na kuzuiwa kwa mali zinazozalisha fedha na pengine kukamatwa kwa wanaohusika endapo watasafiri nje ya nchi.